Breaking News : MTANGAZAJI MAARUFU ISACK GAMBA AFARIKI DUNIA


 Mtangazaji wa Idhaa ya Sauti ya Kiswahili (DW) ya Ujerumani, Isack Gamba amefariki dunia akiwa nchini humo.

Taarifa za awali za kifo cha mtangazaji huyo Mtanzania zinadai amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake leo Alhamisi Oktoba 18, 2018. 

Mmoja wa marafiki zake waliozungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutoka Ujerumani amesema jana Gamba hakuonekana kazini pamoja na juzi Jumanne.

“Hata leo Alhamisi, hakuonekana kazini asubuhi, ndipo tukaamua kwenda kutoa taarifa polisi, waliofika nyumbani kwake na kuvunja mlango wakamkuta Gamba ameshafariki dunia.”

Akiwa nchini, Gamba amewahi kufanya kazi vyombo mbalimbali vya habari ikiwamo Redio Uhuru, RFA, ITV na kabla ya kwenda Ujerumani alikuwa Radio One.

Chanzo- Mwananchi





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527