UZINDUZI WA MFUMO WA KIELETRONI WA KUSAJIRI WAKAAZI WA ZANZIBAR (E-ID CARD)


Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar Dkt. Hussein Khamis Shaban akizingumza na waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali viliko Zanzibar kuhusiana na uzinduzi wa Mfumo wa Uimarishaji wa usajili wa taarifa vitambulisho vya Mzanzibar (ZAN ID) na Ofisi za Wilaya na Mkoa uzinduzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 4-9-2018 katika Wilaya ya Dunga Wilaya ya Kati Unguja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar Dkt. Hussein Khamis Shaban, akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi huo unaotarajiwa kufanyika Wilaya ya Kati Dunga. Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mwanasheria wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar, Hamid Haji Machano akijibu na kutowa ufafanuzi wa maswali yalioulizwa wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari kuhusiana na zoezi la uzinduzi wa usajili wa Vitambulisho vya mzanzibar kwa njia ya kisasa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527