UNLOCK CASTLE LITE YAZIDI KUWAPA RAHA WAKAZI WA JIJI LA DAR


Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakiwa na wateja waliojumuika pamoja katika burudani za furaha ya Castle Lite.

Burudani za furaha ya Castle Lite zikiendelea


Furaha ya Castle Lite ilipamba kila mahali katika kiwanja cha maraha cha 5N kilichopo jijini Dar es Salaam.

Ile promosheni ya kampuni ya TBL kupitia bia yake ya Castle Lite kwa lengo la kuwapatia burudani inayojulikana kama Unlock Castle Lite inazidi kusambaza furaha kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambapo mwishoni mwa wiki ilikuwa kata mti panda mti ndani ya baa ya 5N iliyopo maeneo ya Sinza.

Lengo kubwa la promosheni hiyo ni Kutangaza chapa na kuwashukuru wateja kwa kuendelea kufurahia EXTRA COLD CASTLE LITE!.

Tofauti na promosheni zilizozoeleka, promosheni hii imesheheni kila aina ya burudani ambapo inaweza kuwakutanisha ndugu, jamaa na marafiki pamoja na kupiga picha mbalimbali huku wakifurahia kinywaji bia ya Castle Lite wakiwemo wafanyakazi wa TBL ambao kwa sasa wameamua kutokana ofisini na kujumuika na wateja wao.

Unlock Castle Lite, ambayo inafanyika katika siku za Alhamisi na Ijumaa baada ya saa za kazi pia inawashirikisha wafanyakazi wa kampuni ya TBL ambao wanajumika pamoja na wateja na kuwapatia zawadi mbalimbali za promosheni. Tayari wakazi wa Kawe, Boko na Tegeta, Sinza,wamefikiwa na Unlock Castle Lite.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527