MIILI YA WALIOFARIKI KWENYE KIVUKO YAFIKIA 157

Saa 2:34 Asubuhi Septemba 22

Miili mingine mitano imeopolewa na kufikisha jumla ya miili 21 kwa siku ya Leo na kufanya jumla ya miili 157 iliyoopolewa hadi sasa.


Saa 2:20 Asubuhi, Septemba 22

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela amesema Miili mingine 16 imeopolewa na kufanya jumla ya watu 152 waliofariki dunia kwenye ajali hiyo huku akibainisha kuwa zoezi la uokoaji linaendelea 

Aidha amesema kuwa katika zoezi la utambuzi miili 116 imeshatambuliwa na ndugu zao.

Katika Hatua Nyingine Mongela amesema Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kutolewa kiasi cha shilingi laki tano kwa kila familia ambayo imepotelewa na ndugu yake kwenye Ajali hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527