HUDUMA YA KUJIPIMA UGONJWA KIFUA KIKUU MWENYEWE KWA NJIA YA SIMU YAZINDULIWA TANZANIA

Serikali imezindua huduma za Kifua Kikuu (TB) kwa njia ya mitandao ya simu za mkononi (Mobile Health) ambapo sasa kupitia njia hiyo wananchi wataweza kujichunguza wenyewe iwapo wanakabiliwa na maambukizi ya ugonjwa huo au la.

Aidha, imezindua mfumo wa kusajili na kufuatilia wagonjwa kwa njia hiyo ambao utatekelezwa katika mikoa sita ya Dar es Salaam, Pwani, Kilimanjaro, Arusha, Geita na Mwanza.

Mifumo hiyo imeandaliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) kwa kushirikiana na Path Tanzania/KNCV -challenge TB na Cardno-MHealth PPP Tanzania.

Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, wakati alipokuwa akizindua huduma hiyo mpya ya upimaji.

Alisema hatua hiyo imelenga kuongeza kasi ya uibuaji wa wagonjwa wapya wenye maambukizi ya ugonjwa huo nchini.

Na VERONICA ROMWALD - MTANZANIA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527