AKUTWA NA KICHWA CHA BINADAMU KWENYE UVUNGU WA KITANDA


Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia watu wawili akiwamo mwenye umri wa miaka 65 kwa tuhuma za kukutwa na kichwa cha binadamu nyumbani kwake.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Daniel Shilla akizungumza mjini Chato leo, alisema waliokamatwa ni mkazi wa kijiji cha Ibondo B na mkazi wa Mwabasabhi wilayani Chato.

Alisema tukio hilo lilitokea Septemba 8, 2018 ambapo watuhumiwa hao walikua wamekificha kichwa hicho uvunguni mwa kitanda nyumbani kwa mmoja wao.
Na Rehema Matowo, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527