RADI YAUA WAWILI WAKICHENJUA DHAHABU CHATO


Watu wawili, Benedicto Kalimila (65), mkazi wa kijiji cha Bwanga wilayani Chato na Theodora Charles (62), mkazi wa Kijiji cha Lwamgasa, Geita, wamefariki dunia papo hapo baada ya kupigwa na radi iliyoambatana na mvua.


Kalimila na Charles walikumbwa na mkasa huo katika kijiji cha Lwamgasa wakati wakichenjua mchanga wa dhahabu kwa kutumia karai.

Diwani wa Lwamgasa, Dotto Kaparatus, alisema juzi kuwa, tukio hilo lilitokea Agosti 22, mwaka huu saa nane mchana.

Kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo lilisababisha hisia tofauti kiasi cha ndugu Benedicto kuzuia mwili wa ndugu yao kuondolewa eneo la tukio mpaka kwanza aletwe mganga wa kienyeji ili kuuondolea mkosi pamoja na waliougusa.

Mashuhuda hao, akiwamo Fitina Seleman, ambaye ni mtoto wa marehemu Charles, aliyekuwapo wakati tukio hilo likitokea,walisema radi ilipiga nyumbani kwa Benedicto mara ya kwanza na kuvuunja mti na kupasua ndoo ya plastiki iliyokuwa na maji.

Fitina aliongeza kuwa kwa mara pili radi hiyo ndiyo ilipiga eneo walilokuwapo wote yeye akiwa pembeni na ndipo ilipowapiga wote na Kilamila na Charles walipoteza maisha papo hapo.
Chanzo - Nipashe

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527