Picha : LHRC YAENDESHA MAFUNZO KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA UKATILI WA KIJINSIA KWA WAANDISHI WA HABARI WILAYA YA SHINYANGA

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Centre -LHRC) kimeendesha mafunzo kwa waandishi wa habari wilaya ya Shinyanga yaliyolenga kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya haki za binadamu,jinsia na UKIMWI pamoja na maadili ya uandishi wa habari.



Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika Agosti 27,2018 na Agosti 28,2018 yamefanyika katika ukumbi wa Shinyanga Fairies Motel Mjini Shinyanga.

Akifungua Mafunzo hayo,Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo alisema mafunzo hayo kwa waandishi wa habari za jamii yatawasaidia kuwajengea uwezo kuhusu haki za binadamu lakini pia namna ya kuandika habari kuhusu ukatili wa kijinsia na UKIMWI.

“Mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wetu wa Dreams Innovation Challenge, kwa upande wa waandishi umelenga zaidi kuwawezesha waandishi wa habari kuandika habari zitakazolisaidia kundi la wasichana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 24 waepukane na maambukizi ya VVU”,alisema.

“Mafunzo haya pia yemetolewa kwa makundi mengine muhimu yanayodili na shughuli za watoto ikiwemo vyombo vya dola (Dawati la jinsia polisi), mahakama na watu wa afya,viongozi wa serikali za mitaa ambao wote kwa pamoja wakitimiza wajibu wao watalisaidia kundi hili la wasichana lenye hatari ya kupata maambukizi ya VVU,” aliongeza Kinabo.

Alisema kwa mujibu wa takwimu inaonekana katika eneo la Sahara ya Afrika asilimia 71 ya watoto wanapata maambukizi ya VVU kila siku na chanzo chake ni kufanya mambo kwa kujaribu lakini pia ikiwemo ndoa katika umri mdogo.

ANGALIA PICHA ZA MATUKIO YALIYOJIRI WAKATI WA MAFUNZO HAYO SIKU YA KWANZA NA YA PILI

SIKU YA KWANZA
Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo akifungua mafunzo mafunzo kwa waandishi wa habari wilaya ya Shinyanga yaliyolenga kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya haki za binadamu,jinsia na UKIMWI na maadili ya uandishi wa habari- Picha zote na Kadama Malunde & Michael Mallya
Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo akizungumza wakati wa mafunzo hayo
Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo akitoa mada kuhusu haki za binadamu
Waandishi wa habari wakimsikiliza Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo
Waandishi wa habari wakifurahia jambo ukumbini

Mwanasheria kutoka LHRC Getrude Dyabene akielezea kuhusu mradi wa Dreams Innovation Challenge
Waandishi wa habari wakiwa ukumbini
Waandishi wa habari wakifuatilia mada ukumbini
Mafunzo yanaendelea
Mwezeshaji akitoa mada kuhusu UKIMWI
Waandishi wa habari wakiandika dondoo muhimu
Waandishi wa habari wakiandika dondoo muhimu
Waandishi wa habari wakifuatilia mada ukumbini

ANGALIA PICHA SIKU YA PILI YA SEMINA
Afisa Mawasiliano kutoka LHRC Michael Mallya akitoa mada kuhusu maadili ya uandishi wa habari katika kuandika habari zinazohusu VVU na UKIMWI
Afisa Mawasiliano kutoka LHRC Michael Mallya akiendelea kutoa mada
Afisa Mawasiliano kutoka LHRC Michael Mallya akiendelea kutoa mada wakati wa mafunzo hayo
Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo akitoa mada kuhusu Ukatili wa kijinsia
Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo akisisitiza jambo ukumbini
Mwanasheria kutoka LHRC Theresia Kinabo akielezea nafasi ya waandishi wa habari katika kupiga vita ukatili wa kijinsia 
Mmiliki wa Malunde1 blog,Kadama Malunde akiwa ukumbini
Mwanasheria kutoka LHRC Getrude Dyabene akielezea kuhusu Sheria ya kudhibiti na kupambana na UKIMWI
Mwanasheria kutoka LHRC Getrude Dyabene akifafanua kuhusu haki ya afya
Waandishi wa habari wakiwa ukumbini
Waandishi wa habari wakifuatilia mada ukumbini
Waandishi wa habari wakiwa ukumbini




Picha ya pamoja







Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527