HAWA GHASIA AJIUZULU

 Mbunge wa Kibakwe (CCM), George Simbachawene amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya bajeti leo Jumanne Agosti 28, 2018.

Katika uchaguzi huo, mbunge wa Maswa Magharibi (CCM), Mashimba Ndaki amechaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa kamati hiyo.

Uchaguzi wa viongozi wa kamati hiyo umefanyika baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo, Hawa Ghasia na makamu wake, Jitu Soni.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, Simbachawene amesema mapema leo alihamishwa kutoka kamati ya Bunge ya katiba na sheria kwenda kamati ya bajeti.

Amesema baada ya kuhamishwa na kukuta nafasi ipo wazi, aliamua kugombea uenyekiti na kushinda kwa kishindo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527