PICHA: MWIGULU NCHEMBA AKABIDHI RASMI OFISI KWA KANGI LUGOLA
Tuesday, July 10, 2018
Hatimaye aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Lameck Nchemba, amekabidhi ofisi kwa waziri Kangi Lugola. Makabidhiano hayo yamefanyika mapema leo asubuhi kwenye makao makuu ya wizara hiyo yaliyopo jijini Dodoma.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mwigulu amesema kuwa anamtakia majukumu mema Lugola katika utumishi wake kwa watanzania na kuongeza kuwa mbali na kukabidhi ofisi, amekabidhi pia hotuba ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambayo ina majukumu yaliyopo mbele yake kwa sasa.
“Mbali na ofisi nimekabidhi pia hotuba ambayo ndiyo yenye majukumu ambayo yalikuwa yamepangiliwa kama wizara na serikali katika bajeti hii na kikubwa ni mabadiliko ya baadhi ya sheria zilizokuwa na mapungufu hasa kwa Jeshi la Polisi”, amesema Mwigulu.
Mwigulu ametaja moja kati ya majukumu aliyoacha mezani kuwa ni,kupunguziwa faini kwa madereva bodaboda na bajaji iwe tofauti na madereva wa magari makubwa kwani kuwekwa kwa kiwango sawa ni uonevu kwa madereva hao.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin