MUNA LOVE AMTAJA BABA HALALI WA PATRICK

Ni siku mbili zimepita toka taarifa za kifo cha mtoto wa Muna Love anayejulikana kwa jina la Patrick afariki dunia akiwa Nairobi nchini Kenya akipatiwa matibabu ambaye alifariki July 3,2018.

Baade taarifa zilienea kuhusiana na Peter Zacharia Komu aliyejitokeza na kudai ni baba mzazi wa Marehemu Patrick na kutaka msiba ufanyike nyumbani kwakwe Mwananyamala huku taarifa nyingine zikidai baba wa mtoto ni mtangazaji wa Clouds Tv Casto Dickson.

Kupitia instagram account ya Munalove amefunguka kuhusiana na mvutano ambao umekuwa ukiendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na baba mzazi wa marehemu Patrick.

“Jaman jamani 😭😭😭😭😭😭 naomba nimzike mtoto wangu 😭😭😭😭 vaeni viatu vyangu. Kuna siri kumbwa amjawahi kuijua nawaomba nimzike mtoto wangu alafu ndiyo mnitukane. Mimi 😭😭😭😭😭😭 naumia jamani, namuheshimu Peter siwezi kuweka kitu hapa maana nitamwaibisha….

"Siwezi kumsema Casto maana yeye anajua wapi alikosea, nawaombeni jamani, naomba nataka kumzika mwanangu. Miaka miwili nahangaika na Paty wangu 😭😭😭😭😭😭😭😭, nimalize kumzika niongee.

"Nyie wanawake mnaonihumuku, vaeni viatu vya siri nilizohifadhi… baba wa mtoto ni Casto, inatosha 😭😭😭😭😭😭😭😭, nitukaneni mimi nife ila Paty ni kiongozi alieniongoza nione maisha mapya na nimjue Mungu… Nitalia milele mimi.

"Paty wangu😭😭😭😭😭😭😭😭leo wanakugombania mwaanangu, natamani urudi mara moja😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭… Mwanangu ntaleta ijumaa na ntamzika Jumamosi😭😭😭😭😭, msiba uko kwangu Mbezi Beach.” amesema Muna. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527