WAZIRI MKUU AZINDUA KITUO CHA AFYA CHA MWENDAKULIMA KILICHOJENGWA NA MGODI WA BUZWAGI - KAHAMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mwendakulima wilayani Kahama, Julai 15, 2018.  Kituo hicho kimejengwa kwa hisani ya mgodi wa Buzwagi wialayani Kahama.Wa pili kushoto ni Mbunge wa Kahama, Jumanne Kishimba, Kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Stanslaus Nyongo na wapili kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kakunda. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa ACACIA, Asa Mwaipopo. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amembeba mtoto aliyepewa jina la Majaliwa ambaye ni mmoja wa watoto waliozaliwa katika Kituo cha Afya cha Mwendakulima kilichopo Kahama baada ya kukizindua kituo hicho Julai 15, 2018. Kituo hicho kimejengwa  kwa hisani ya mgodi wa Buzwagi. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimbeba mmoja wa watoto waliozaliwa katika Kituo cha Afya cha Mwendakulima baada ya kukizindua kituo hicho kilichojengwa na Mgodi wa Buzwagi wilayani Kahama Julai 15, 2018. Wapili kulia ni mama wa mtoto huyo  aliyepewa jina la Majaliwa, Leticia Elias na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.  Kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kakunda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527