USWIZI YAICHAPA SERBIA 2- 1 DAKIKA ZA MAJERUHI

Switzerland imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Serbia katika mchezo wa kundi E

Mabao ya mchezo huo yalifungwa na Mitrovic mnamo dakika ya 5 tu ya mchezo kwa upande wa Serbia huku la Switzerland likiwekwa kimiani na Granit Xhaka mnamo dakika ya 52 kabla ya Xherdan Shaqiri kuongeza msumari wa mwisho dakika ya 90 ya mchezo

Xhaka ambaye hivi karibuni amesaini mkataba wa muda mrefu kuitumikia Arsenal ameweka rekodi ya kupiga jumla ya pasi 71 ambazo hazijapigwa na mchezaji yoyote wa Urusi katika michuano hiyo tangu 1996.

Matokeo hayo yanaifanya Uswizi kuwa pointi sawa na Brazil katika kundi E lakini ikishika namba 2 kutokana na idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527