HUU NDIYO MJI AMBAO MTU HARUHUSIWI KUFA

Eneo la Mji wa Longyearbyen nchini Norway

Mji wa Longyearbyen nchini Norway ndio mji pekee ambao mtu haruhusiwi kufa kwa sababu akifa mwili wake hautaharibika kutokana na eneo hilo kuwa hali ya hewa ya baridi hivyo mwili utabaki na kukaribisha wanyama.


Wakazi wa eneo hilo wanaamini kuwa kutoharibika kwa miili kutawavutia Wanyama wakali wa katika mji wao hivyo kuhatarisha usalama wao.

Hivyo kutokana na sababu hiyo wakazi wa eneo hilo ambao wanaonekana kukaribia kufa, huondolewa katika mji huo na kupelekwa miji mingine na shuguli nzima ya mazishi humalizikia kule.

Katika mji huo kuna eneo la makaburi ambalo halijawahi kutumika toka mwaka wa 70 sasa, na Joto linaweza kuwa chini ya nyuzi -46.3 .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527