ARGENTINA NA URENO WAMETUPWA NJE KOMBE LA DUNIA....MESSI,RONALDO KWISHAAA

 Mbappe akimpa pole Messi

Ronaldo

Kombe la Dunia 2018 limekuwa bila huruma kwa mastaa wawili wa soka waliotawala kizazi chao, Lionel Messi wa Argentina na Cristiano Ronaldo wa Ureno baada ya wawili hao kung'olewa ngarambe hizo hatua ya muondoano.


Kutokana na hali hiyo,ukurasa mpya umefunguliwa kwa mashabiki wa soka duniani kuhusu ubora wa wachezaji maarufu wa soka.

Ingawa kila mwamba ngoma, ngozi huivutia kwake, ukweli ni kuwa, wachezaji wapya wametumia vyema jukwaa lililopatikana Kombe la Dunia Urusi 2018.

Baada ya kutawala vinywa vya wengi ndani ya zaidi ya kipindi cha miaka 10, kuondoka kwa Argentina na Ureno Urusi hatua za mchujo, imewanyima Messi na Ronaldo muda zaidi wa kujadiliwa.

Kurunzi za soka sasa zimeelekezwa kwa Neymar wa Brazil, Paul Pogba, Kylian Mbappe na Antoine Griezmann wa Ufaransa, Edison Cavani na Luis Suarez wa Uruguay, Harry Kane wa Uingereza na Romelu Lukaku wa Ubelgiji.

Orodha ni ndefu, lakini yote yataamuliwa kulingana na mchango wa wachezaji hawa kwa ufanisi wa timu zao.

Kuondoka kwa Ureno imekuwa pigo la kipekee kwa Ronaldo, aliyejitahidi kuzidisha mabao yake Urusi kwani ni wazi sasa wenzake watampiku kwenye uwaniaji wa tuzo ya mfungaji bora.

Ronaldo, alianza vyema baada ya kuondoka na mpira wa mechi dhidi ya Uhispania alipofunga hat-trick mechi yake ya kwanza.

Kipa wa Iran Ali Beiranvand pia alimnyima kwa kushika penalti yake walipokutana.

Kwa sasa mbio ni kati ya Lukaku, Harry Kane, Cavani na Mbappe na wengine.

Diego Costa wa Uhispania na Cheryshev wa Urusi watapata fursa ya kufunga mabao wawili hao watakapokwaruzana siku ya Jumapili katika uwanja wa Luzhniki, Moscow.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527