Hayo yamesemwa leo Mei 2, 2018 Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Tamisemi, Joseph Kakunda wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Ludewa (CCM), Deogratius Ngalawa.
Katika swali lake, Ngalawa alitaka kupata majibu ya Serikali kuhusu upungufu wa walimu 500 wa shule za msingi na jinsi litavyoshughulikiwa.
Akijibu swali hilo, Kakunda amesema; "Tunaendelea na mchakato kwa kushirikiana na Baraza la Mitihani la Taifa kwa kupitia vyeti vya vya walimu na tunategemea ifikapo Juni 30 kuwaajiri."