MBUNGE LEMA AMSHANGAA RC GAMBO KUMUITA RAFIKI....'HAKUOGOPA KUWA MUONGO MADHABAHUNI'

Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema hajasita kuweka wazi hisia zake baada ya kutambulishwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katika Ibada ya kusimikwa Mhashamu Isaack Amani kuwa Askofu Mkuu Jimbo la Katoliki la Arusha.


Lema kupitia ukurasa wake wa Twitter ameonekana kushangaa kitendo cha RC Gambo kumuita yeye rafiki.


Ameandika; “Katika Ibada ya kusimikwa Askofu, Rais aliongea neno la Mungu kuhusu Amani na Haki. Bila shaka demokrasia na haki vitashamiri tena. Askofu Amani yeye akasisitiza ushirikiano kisiasa bila kubaguana. Mrisho Gambo(RC) yeye hakuogopa kuwa muongo madhabahuni, eti aliniita Mimi rafiki yake."

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527