Watahiniwa hao 29 wamefanya hivyo wakifuata nyayo za watangukizi wao 35 waliofanya mitihani kama hiyo mwaka jana waliopeleka msaada kama huo na kujikuta wakipata ufaulu wa kuwawezesha wote kupata mkopo wa Serikali katika vyuo vikuu walivyochaguliwa.
Wakizungumza wakati wakikabidhi msaada huo watahiniwa hao wamesema licha ya kwamba walimu wao wamefanya kazi ya ziada kuwafundisha itakayohakikisha wanafanya vyema mitihani ya kujiunga na elimu ya juu lakini baraka za wazee hao waathirika wa ukoma zina umuhimu wa aina yake.
“Tumekuja hapa tukiamini kwamba wakifurahi wazee hawa kwa ajili yetu watatupa baraka za kutuwezesha kufanya vyema mitihani ya Taifa ya kidato cha sita na kwenda vyuo vikuu wote”amesema Shedrack Mnzava ambaye ni kiongozi wa wanafunzi hao wa kidato cha sita.
Msaada waliotoa wanafunzi hao ni mikate,nyembe,wavu wa mbu wa kuweka madirishani,sembe sukari,sabuni pamoja na simu vyote vikiwa na thamani ya sh 500,000.
Na Burhani Yakub,Mwananchi
Social Plugin