RAIS SHEIN AFANYA MABADILIKO KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI ZANZIBAR..ANGALIA HAPA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mapinduzi kwa kuongeza Wizara moja zaidi, na kuwabadilishia Wizara baadhi ya Mawaziri.
 
Kufuatia mabadiliko hayo, shughuli za Vijana zimehamishiwa katika Wizara mpya ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo; shughli za Mazingira zimehamishiwa katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais; na shughli za Wakala wa Serikali wa Uchapaji zimehamishiwa Wizara mpya ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale.
 
Aidha, amewateua Naibu Mawaziri wapya wawili na kumbadilisha Wizara Naibu Waziri mmoja. Kufuatia mabadiliko hayo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hivi sasa itakuwa na Wizara 14 zenye Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:
  1. OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI
  2. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi- Mheshimiwa Issa Haji Ussi Gavu
  3. OFISI YA RAIS, KATIBA SHERIA, UTUMISHI WA UMMA NAUTAWALA BORA
  4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mheshimiwa Haroun Ali Suleiman
  5. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mheshimiwa Khamis Juma Mwalim
  6. OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ
  7. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ – Mheshimiwa Haji Omar Kheri
  8. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ – Mheshimiwa Shamata Shaame Khamis
  9. OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS
  10. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed
  11. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mheshimiwa Mihayo Juma Nhunga
  12. WIZARA YA AFYA
  13. Waziri wa Afya- Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed
  14. Naibu Waziri wa Afya – Mheshimiwa Harusi Said Suleiman
  15. WIZARA YA ARDHI, NYUMBA, MAJI NA NISHATI
  16. Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati – Mheshimiwa Salama Aboud Talib
  17. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati – Mheshimiwa Juma Makungu Juma
  18. WIZARA YA BIASHARA NA VIWANDA
  19. Waziri wa Biashara na Viwanda – Mheshimiwa Balozi Amina Salim Ali
  20. Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda – Mheshimiwa Hassan Khamis Hafidh
  21. WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
  22. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali – Mheshimiwa Riziki Pembe Juma
  23. Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amal Mheshimiwa Mmanga Mjengo Mjawiri
  24. WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
  25. Waziri wa Fedha na Mipango – Mheshimiwa Dkt. Khalid Salum Mohamed
  26. WIZARA YA HABARI, UTALII NA MAMBO YA KALE
  27. Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo
  28. Naibu Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Choum Kombo Khamis
  29. WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI, WAZEE, WANAWAKE NA WATOTO
  30. Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto – Mheshimiwa Maudline Cyrus Castico
  31. Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto – Mheshimiwa Shadia Mohamed Suleiman
  32. WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI
  33. Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi – Mheshimiwa Rashid Ali Juma
  34. Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi – Mheshimiwa Dkt. Makame Ali Ussi
  35. WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI
  36. Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji – Mheshimiwa Dkt. Sira Ubwa Mamboya
  37. Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji – Mheshimiwa Mohamed Ahmada Salum
  38. WIZARA YA VIJANA, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
  39. Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo – Mheshimiwa Balozi Ali Abeid Karume
  40. Naibu Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo – Mheshimiwa Lulu Msham Abdulla
Aidha, Mheshimiwa Said Soud Said na Mheshimiwa Juma Ali Khatib wanaendelea kuwa Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalum.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527