MWENYEKITI WA MTANDAO WA WANAFUNZI TANZANIA ALIYEPOTEA ATUPWA IRINGA

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania , Abdul Nondo ambaye pia ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) aliyeripotiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha amepatikana akiwa hai eneo la Mafinga mkoani Iringa.


Imeelezwa kuwa, Nondo alijikuta katika eneo hilo baada ya kuzinduka kutoka katika lindi la usingizi na kuwauliza wenyeji wa eneo hilo kuwa hapo ni wapi? Wenyeji hao walimfahamisha kuwa yuko Mafinga mkoani Iringa na kisha akapelekwa katika kituo cha polisi kilichoko karibu.


Polisi walifanya mahojiano na mwanafunzi huyo ili kuweza kujua nini hasa kilitokea na baada ya hapo kupiga simu kwa ndugu zake.


Baada ya Baba mzazi, Mussa Mitumba kupata taarifa za kuonekana kwa mwanae, aliomba namba za askari aliyemfanyia mahojiano ili kujua nini kilimpata mwanae aweze kujua kama jambo jingine alilowaambia kuhusiana na kupotea kwake.


Awali kabla ya tukio hilo mwanafunzi huyo alielezea kwamba alikuwa akifuatiliwa mara kadhaa watu asiowatambua

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527