Na Rhoda Ezekiel- Malunde1 blog
Mkurugenzi wa Shirika la utangazaji TBC Dr. Ayoub Rioba amepata ajali ya gari katika kijiji cha Mgombe kata ya Nyakitonto wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wakitokea wilayani Kibondo kuelekea mjini Kigoma.
Akizungumza leo Jumanne Machi 20,2018 mara baada ya tukio hilo kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Kigoma Martine Otieno amesema ajali hiyo pia imesababisha vifo vya watu wawili.
Aliwataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni watembea kwa miguu wawili waliofahamika kwa majina ya Teresia Mpoma (55) mkulima na Mkazi wa Nyakitonto na Yuster Masharubu (55) mkazi wa Nyakitonto.
Ajali hiyo pia imesababisha majeruhi mmoja aliyefahamika kwa jina la Diana Shedrack (10) mwanafunzi shule ya Msingi Nyakitonto ambaye hali yake ni mbaya na anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu.
Alisema katika ajali hiyo waliokuwemo kwenye gari ni Mkurugenzi wa Vipindi TBC Dr. Ayoub Rioba na Meneja wa vipindi kanda ya Magharibi Zabron Mafuru na dereva aliyefahamika kwa jina laAbubakari ambapo wao wamepata majeraha madogo madogo na wamepatiwa matibabu na wanaemdelea vizuri.
Kamanda Otieno alisema chanzo cha ajari hiyo ni utelezi unaotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo na kuwaomba madereva kuendesha magari kwa umakini kutokana na ubovu wa barabara hiyo na kuzingatia sheria za barabarani.
Muonekano wa gari baada ya ajali hiyo
Kushoto ni Dr. Ayoub Rioba