MASHEIKH WALIOPOTEA ZANZIBAR WAPATIKANA


Masheikh watano waliotekwa na watu wasiojulikana katika mazingira ya kutatanisha visiwani Zanzibar, hatimaye wamepatikana.

Kiongozi wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar, Amir Haji Khamis Haji na wenzake wanne waliotoweka Februari 9, mwaka huu, waliachiwa juzi na kuungana na familia zao.

Akizungumza baada ya kuachiwa na watu hao, Amir Haji, alisema baada ya kukamatwa na watu hao, alifungwa kitambaa usoni na kupelekwa asikokujua na watu hao wasiojulikana.

“Binafsi siwajui hata waliofanya hivyo, lakini hadi leo hii (juzi) kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu milango ya asubuhi saa tano na nusu, naona nimeachiwa huru bila kuwa na madhara yoyote ikiwemo kuuawa.

“Na sasa niko nyumbani ni mzima, sikupata athari ya kupigwa na kitu chochote, kwahiyo nawaomba Waislamu wote waridhike na hilo, tuwe pamoja na waniombee dua mzee wao, hakuna kilichoharibika.

“Tuendelee na tuko pamoja na tuhifadhi mambo ya baadaye Inshallah. Sikuulizwa maswali yoyote, naona wao walikuwa wakifanya kazi yao, nasi kwa upande wa dini tunafanya pia.

“Kitu muhimu ni kuangalia masilahi ya baadaye na kuweka amani na hawa waliofanya haya nafikiri walikuwa wakifanya haya kwa ajili ya kuweka amani,” alisema Amir Haji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527