MANGE KIMAMBI AMMWAGIA POVU WEMA SEPETU KISA DIAMOND

Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi ameibuka na kumwagia matusi mazito msanii wa Bongo movie Wema Sepetu baada ya kuzua maneno maneno jana kwenye mtandao wa Instagram.


Siku ya jana Wema alishika headlines za mitandao ya kijamii baada ya kuposti posti kadhaa zilizoamsha tetesi kuwa amerudiana na Diamond na alizidi kuzua maneno baada ya kuonekana akiwa na Esma huku wakiitana wifi.


Sio siri kuwa Wema na Mange wapo kwenye bifu kali tangu Wema afanye uamuzi wa kurudi CCM mapema mwaka jana akitokea Chadema na hata kuanzisha urafiki na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam jambo ambalo halikumfurahisha Mange.

Siku ya jana Mange amemtolea povu zito Wema na kumtuhumu anatumika kuleta drama zake na Diamond ilimradi wazime amsha amsha za maandamano na kudai amegeuzwa Jinga na familia ya Diamond.

Kupitia ukurasa wake Instagram, hili ndio povu la Mange kwa Wema:

"...........Wema mj***ga sana, mtu gani kutwa anatafuta attention za watu kwa mambo ya kijinga? Forever my wii my foot mbona Bi. Tukinao alivyokuwa nao mbona hawakukuita forever my wii? 

"Yamewashinda kwa mganda ndio wamelikumbuka jinga lao. Janamke j*nga halikui from CEO wa Endless Fame to mfanyakazi wa Wasafi Tv? 

"Seriously wenzake wanasonga mbele lenyewe linarudi nyuma. Halafu hata halijistukii linaongea proudly kabisa “Sasa Diamond anaenda kuwa bossi wangu” from kuwa CEO mpaka kuwa mfanyakazi wa Diamond kama wakina Kifesi?”.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527