MAABARA YA KISASA YA TFDA KANDA YA ZIWA KULETA AHUENI KWA WANANCHI


Wafanyabiashara wakiwemo wazalishaji wa bidhaa mbalimbali Kanda ya Ziwa, wametakiwa kuitumia vyema Maabara ya Kisasa ya Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA iliyopo Jijiji Mwanza ili kufanya uchunguzi wa bidhaa zao kabla ya kuziingiza sokoni.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.Mpoki Ulisubisya aliyasema hayo jana baada ya kufanya ziara ya kukagua ufungwaji wa mashine za maabara hiyo, kujionea utendaji pamoja na kuzungumza na wafanyakazi wa TFDA.


Kaimu Mkurugenzi Mkuu TFDA, Agnes Kijo alisema uwepo wa maabadara ya hiyo Kanda ya Ziwa, utasaidia uchunguzi wa bidhaa mbalimbali kukamilika kwa wakati na hivyo kuwaondolea usumbufu wazalishaji wa bidhaa hizo wakiwemo wenye viwanda vidogo vidogo.

Serikali kwa kushirikiana na taasisi ya Global Fund imefanikisha upatikanaji wa mashine za kisasa katika ofisi za TFDA Kanda ya Ziwa pamoja na Makao Makuu vilivyogharimu zaidi ya shilingi bilioni tano.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527