DENI LA TAIFA LAPAA HADI TRILIONI 46 ..CAG ATOA TAHADHARI KWA SERIKALI YA TANZANIA

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad amesema deni la Taifa linatia wasiwasi hivyo Serikali inatakiwa kuchukua hatua kupunguza ukubwa wa deni hilo.


Profesa Assad ametoa kauli hiyo leo Jumanne Machi 27, 2018 na kubainisha kuwa deni hilo ni Sh46 trilioni kutoka Sh41 trilioni la mwaka uliopita, kwamba ni ongezeko la asilimia 12.


Ametoa kauli hiyo leo Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa uwasilishaji wa ripoti yake ya ukaguzi mwaka 2016/17 iliyobaini madudu Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma.


“Tulichosema hapa kwa kweli ukuaji wa deni tunasema ni himilivu lakini jinsi linavyoongezeka tunakaribia maeneo ya wasiwasi. Asilimia 72 ya GDP (Pato la Taifa) siyo mbaya lakini ikifika asilimia 76 nchi nyingine zimepata shida, inabidi tuangalie sasa namna gani tunaweza ku-control ukuaji wa deni hilo,” amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527