WAPENDANAO WA TATU MZUKA WAZIDI KUJIZOELEA MAMILIONI



Msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la Aslay akimhoji mmoja wa wapendanao Mwanaidi Msangi ambaye alikuwa ni mmoja kati ya Washindi na Mpenzi wake Kelvini Gibson pichani kulia.Wakazi hao wa Buguruni malapa walijinyakuliwa milioni kumi na kugawana kila mmoja milioni tano,kulia ni msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la kisanii Nandy
Kulia ni msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la kisanii Nandy akimhoji  mmoja wa wapenda nao Kelvini Gibson,wakazi wa Buguruni Malapa  waliojinyakuliwa milioni tano tano kwa kila mmoja mwishoni mwa wiki,katika kushiriki kampeni ya Wapendanao ilionzishwa na mchezo huo wa kubahatisha wa Tatu Mzuka,uliobeba kauli mbiu iliyojulikana kwa jina la 'Ukishinda na umpendae anashinda' ,kushoto ni Msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina Aslay
Pichani kati ni Wawili wapenda nao Mwanaidi Msangi pamoja na Kelvin Gibson wakiwa sambamba katika picha ya pamoja huku wakiwa wameshika mfano wa hundi ya shilingi milioni Kumi waliojishindia kwenye muendelezo wa kampeni ya Wapendanao ilioanzishwa na Tatu Mzuka, Kulia ni msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la  kisanii Nandy pamoja na Msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la Aslay,ambao kwa pamoja wanatarajiwa kutumbuiza jumamosi hii katika ufukwe wa kiota cha maraha cha Escape One,Mikocheni jijini Dar es salaam.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527