DANCER WA DIAMOND PLATNUMZ AWATEMBEZEA KICHAPO SHILAWADU

Watangazaji wa Kipindi maarufu cha Shilawadu kinachorushwa na Clouds tv,Soudy Brown na Kwisa wamechezea kichapo kutoka kwa Dancer wa Diamond,Mose Iyobo,usiku wa kuamkia  ijumaa,baada ya kutaka kumuhoji kuhusu matukio yaliyotokea hivi karibuni kati ya familia yake na mwanadada Tunda.

Wakithibitisha kutokea kwa tukio hilo,Shilawadu wameandika katika ukurasa wao wa instagram:

Kazi yetu ina changamoto kubwa sana..asilimia kubwa ya ma star wanatuunga mkono.

Usiku wa Leo wakati tukiwa kazini tumenusurika kumwagwa damu na mtu tuliemfuata kumuomba kufanya naye mahojiano,kati yetu kuna walioumia viuno,mikono, etc.kuna uharibifu wa vifaa vyetu vya kazi umetokea pia,wenzetu wanaendelea na matibau Mungu  ni mwema  Mungu ni wetu sote na hili litapita bado tuna wasiwasi tu kama mhusika ataendelea kututafuta kwa ajili ya kutudhuru zaidi,tunasikitishwa sana na matumizi ya nguvu dhidi yetu sisi Wanyonge #Shilawadu

Kuna watu watasema Shilawadu wamezidina kusahau kuwa sisi ni wana Habari kama wanahabari wengine na kupata habari ni haki ya kila mwananchi kama ilivyo haki nyingine yoyote ile.Kifungu cha 18 cha katiba  ya Jamhuri ya Muungano 1977 na hatimaye kufanyiwa marekebisho mwaka 2005 inampa haki mtu na uhuru wa kujieleza na kutoa mawazo,uhuru wa kutafuta habari,kupata habari,na kuneza habari bila kujali mipaka,pia sheria hiyo inampa haki mtu ya kuwasiliana bila kubughudhiwa na mawasiliano na kufahamishwa wakati wowote masuala yoyote muhimu yahusuyo maendeleo yake na yahusuyo jamii yake kwa ujumla.
 
Imeandikwa na Mtayarishaji wa Kipindi cha Shilawadu Benedict Noel


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527