UVCCM WAUNDA YAUNDA KAMATI KUFUATILIA VITEGA UCHUMI NA MALI ZAO




Umoja wa Vijana UVCCM, umeunda kamati ya kufuatilia vitega uchumi na mali za umoja huo nchi nzima. 

Kamati hiyo inaundwa na wajumbe nane na itaongozwa na Mariam Chaurembo.


Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka amesema kamati hiyo inakwenda kuchunguza na kuangalia vitega uchumi na mali zote za umoja huo.


"Mwenyekiti ameanza na kazi hii ili aweze kujua mali na vitega uchumi na umoja viko katika hali gani na vinaendeshwaje,"


"Wajumbe hawa watafanya kazi hiyo kuanzia leo wakiangalia na kufuatilia, kuchunguza, kuorodhesha mali za chama na mapato yanayotokana na vitega uchumi hivyo zinakwenda wapi," amesema Shaka


Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Peter Kasera, Zelote Saitoti, Rose Manumba, Sofi Kizigo na Elly Ngowi. Shaka amesema wajumbe wengine wawili watateuliwa kujiunga na kamati hiyo ambayo inaanza leo.

Na Elizabeth Edward,Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527