MAMA WEMA SEPETU AMTEMBELEA TUNDU LISSU NAIROBI

Mama Mzazi wa msanii wa filamu Bongo na Mkurugenzi wa Endless Fame, Wema Sepetu wameenda Nairobi nchini Kenya kumjulia hali mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu ambaye anapata matibabu nchini huyo.


Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amekuwa akitibiwa Nairobi tangu aliposhambuliwa kwa kupigwa risasi September mwaka huu. 


Viongozi mbali mbali wa kiserikali na wa chama hicho wamekuwa wakienda kumjulia hali na sasa Mama wa Wema Sepetu ameonekana kufanya hivyo.


Hapo jana Makamu wa Rais Mhe. Mama Samia Suluu alimtembelea pia Lissu hospitalini hapo. Mama Wema pamoja na mwanaye February 24 mwaka huu walitangaza kujiunga na Chadema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527