MAMA SAMIA : NAPIGA GOTI MBELE YA MUME WANGU KUONESHA MAPENZI NA HUBA

Makamu wa rais Samia Suluhu Hassan, amesema pamoja na wadhfa alionao, lakini mbele ya mume wake atapiga goti ili kuonesha mahaba aliyonayo kwake.


Mheshimiwa Samia Suluhu alitoa kauli hiyo jana Septemba 5,2017 wakati akizindua tamasha la 14 la Jinsia mwaka 2017 lilirotaribiwa na TGNP Mtandao na Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia (GTI) katika Viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam lenye mada kuu isemayo “ Mageuzi ya Mifumo Kandamizi Kwa Usawa wa Kijinsia na Maendeleo Endelevu”.


Alisema wanawake hawako sawa katika nyanja zote za kijamii na wanatakiwa kutunza mila na desturi nzuri, na kuelezea kuwa hapigi goti kwa mume wake kwa sababu ni mdhaifu 'inferior' ila ni kuonyesha mapenzi na huba.

"Tushirikiane bila kuacha mila na desturi zetu nzuri,tuende na wanaume katika kuleta maendeleo yetu...hatuko sawa katika nyanja zote za kijamii,mimi na umakamu wangu wa rais mbele ya mume wangu nitapiga goti,na sipigi goti kwamba ni Inferior,hapana!,napiga goti kwa sababu ya huba na mapenzi"..Samia Suluhu.

MSIKILIZE HAPA AKIZUNGUMZA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527