News Alert: MAHAKAMA KENYA YAFUTA USHINDI WA RAIS UHURU KENYATTA....FUATILIA HAPA MATANGAZO LIVE




Mahakama ya juu nchini Kenya imefuta ushindi wa Rais Uhuru Kenyata kwa uchaguzi uliofanyika Agosti 8, 2017, na kutaka uchaguzi huo urudiwe.

Hukumu hiyo imetolewa leo na jopo la majaji 6 ilirushwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari nchini Kenya, imesema uchaguzi huo utarudiwa baada ya siku 60. 

Akisoma uamuzi huo Jaji Mkuu David Maraga amesema tume ya uchaguzi ilikiuka Katiba na Sheria katika baadhi ya mambo na hivyo kuathiri matokeo ya uchaguzi. 

"Uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8 mwaka 2017, haukuandaliwa kwa mujibu wa katiba na sheria hivyo matokeo yake ni batili. Natangaza kwamba Bw Kenyatta hakuchaguliwa na kutangazwa kwa njia inayofaa, agizo linatolewa na kuagiza Tume ya Uchaguzi kuandaa na kufanyisha uchaguzi mwingine kwa kufuata katiba na sheria katika kipindi cha siku 60", alisema Jaji Maraga.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post