HALIMA MDEE AGOMA KWENDA KWA DCI

Mbunge wa jimbo la Kawe jijini Dar es salaa Halima James Mdee amesema hajaenda kuripoti kwa DCI kama ilivyotakiwa kwa sababu yeye hajaitwa rasmi.


Mdee amesema DCI ametoa tangazo la ujumla, lakini yeye binafsi hajapewa wito wowote, hivyo hawezi kwenda kutokana na taarifa hiyo.


"Mimi nimesikia tangazo la ujumla, wakiniita in personel Halima njoo nitaenda na hakuna popote kwenye kauli yao iliposema Halima Mdee njoo, lakini siwezi kwenda kwa 'general statement', amesema Halima Mdee


Juzi Jeshi la Polisi liliwataka watu wote waliopost kwenye mitandao ya kijamii kuhusu askari wao aliye nchini Nairobi wakimuhusisha na kumfuatilia Tundu Lissu nchini Kenya kwenye matibabu na kutakiwa kuripoti wenyewe kwa DCI, kabla ya kitengo cha sheria za makosa ya mtandaoni hakijawachukulia hatua zaidi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527