WATU SABA WAFARIKI KWA AJALI

N:B Picha haihusiani na habari hapa chini

Watu saba wamefariki katika ajali mbili tofauti ambapo ajali ya kwanza watu wawili wa familia moja wamepoteza maisha na wengine sita kujeruhiwa katika ajali ya gari dogo aina ya Kluger iliyotokea eneo la Masaki mkoani Pwani leo.


Majeruhi sita wa ajali ya gari ndogo iliyotokea mkoani Pwani wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani na taratibu zinafanyika ili kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi kutokana na hali zao kuwa mbaya.


Aidha watu wengine watano wamefariki dunia na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha lori la mzigo lililokuwa limebeba abiria mkoani Singida.


Ajali zote mbili zimesababisha vifo vya watu saba huku wengine 26 wakiwa ni majeruhi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527