POLISI AMNUNULIA MWIZI NGUO ALIZOKAMATWA NAZO AKIZIIBA DUKANI

Mwizi wa duka huko Toronto ambaye alishikwa akiiba nguo ili aweze kuivaa kwa usaili alipata fusra asiyoitarajia kutoka kwa polisi ambaye aliitwa kuja kumkamata.

Niran Jeyanesan aliambia kituo cha habari cha CP24 kuwa mfanyakazi wa duka la Walmart, aliripoti kuwa mtu huyo wa umri wa miaka 18 alijaribu kuiba shati, tai na soksi.

Alisema kuwa wakati alifika eneo hilo aligundua kuwa mtu huyo alikuwa akiiba nguo ili avae akienda kufanyiwa mahojiano ya kutafuta ajira.

Hapo ndipo aliamua kumuachilia na kumnunulia nguo hizo.

"Kijana huyu amekuwa akikumbwa na wakati mgumu maishani na anajaribu kutatua hilo kwa kuitafutia familia yake riziki kwa kujaribu kupata kazi," bwana Jeyanesan alisema.

Akiongea na BBC mkuu wa Jeyanean, Paul Bois alipongeza kitendo hicho chake.

Chanzo- BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post