MBUNGE HALIMA MDEE ATINGA MAHAKAMANI TENA..KESI YAAHIRISHWA HADI SEPTEMBA 12


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kupitia kwa Mawakili wake amewasilisha pingamizi la awali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi yake ya kumtolea lugha chafu Rais Magufuli.

Mawakili watano wa Halima Mdee, wakiongozwa na Hekima Mwesigwa wamewasilisha pingamizi hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa baada ya Wakili wa Serikali Leonard Chalo kudai shauri hilo limekuja kwa ajili ya kitajwa.

Mwesigwa amedai kuwa wana mapingamizi mawili, kwanza hati ya mashtaka ina mapungufu, pia Mahakama hiyo haina mamlaka akisema kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka kwa sababu, Mkuu wa Wilaya aliyetoa amri ya kukamatwa kwa Mdee ameshindwa kufuata matakwa ya kisheria.

Baada ya kueleza hayo kesi hiyo imeahirishwa hadi September 12, 2017.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post