KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AMUAGA KWA CHAKULA BALOZI WA CHINA


Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkabidhi zawadi maalum Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing, wakati wa  hafla ya Chakula cha jioni alichomwandalia Balozi huyo kumuaga, Upanga  jijini Dar es Salaam, jana Agosti 25, 2017. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo, Naibu Spika Tulia Akson, Mabalozi kadhaa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, Mawaziri Kadhaa, Makatibu wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa na Makatibu wa Jumuia za Chama. Picha zote na Bashir Nkoromo.
Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing akimshukuru Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana baada ya kupokea zawadi maluum, ambayo Kinana alimzawadia wakati wa chakula cha jioni alichomwandalia Balozi huyo kumuaga.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza kabla ya kumkabidhi zawadi maalum Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing (kulia), wakati wa  hafla ya Chakula cha jioni alichomwandalia Balozi huyo kumuaga, Upanga  jijini Dar es Salaam
Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing (kulia) akiifungua zawadi hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing (kulia) akizungumza wakati wa hafla hiyo. 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na 
Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing wakiinua glasi za vinwaji kabla ya kuzigonganisha kutakiana heri, wakati wa 
hafla ya Chakula cha jioni alichomwandalia Balozi huyo kumuaga, Upanga jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Spika wa Bunge
Tulia Akson. 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akigonganisha glasi za vinywaji na  Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing kumtakia heri, wakati wa hafla ya Chakula cha jioni alichomwandalia Balozi huyo kumuaga
Balozi wa China nchini Tanzania Dk. Lu Youqing akigonganisha glasi za vinywaji na Spika wa Bunge Tulia Akson kutakiana her, wakati wa hafla ya  Chakula cha jioni kilichoandaliwa na katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman  Kinana kumuagaBalozi huyo, Upanga jijini Dar es Salaam,jana Agosti 25, 2017. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uratibu wa Bunge
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akigonganisha glasi za kinywaji na Waziri Jenista Mhagama wakati wa hafla hiyo. Kushoto ni Balozi Lu na wapili kulia ni Naibu Spika Tulia Akson.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo akigonganisha Glasi na Balozi wa Zambia hapa nchini Judith Kangoma-Kapijimpanga wakati wa hafla hiyo. 
Katibu wa Jumuia ya wanawake Tanzania Amina Makilagi, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Idara ya Uchumi na Fedha Dk. Frank Hawassi na kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka hamdu Shaka wakiwa na glasi za vinywaji vyao wakati wa hafla hiyo. KWA PICHA NYINGI ZA HAFLA HIYO/BOFYA HAPA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post