AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUJIFANYA MKURUGENZI WA HABARI WA IKULU

Mfanyabiasha Ramadhani Athumani Juma maarufu kama Elias Jeremiah Mazimbaka amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na shtaka la kujitambulisha kuwa yeye ni Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu, Gerson Msigwa.


Amesema hati ya mashtaka jana wakili wa Serikali, Jacqline Nyantori alidai kuwa kati ya Juni 28 na Julai 4,2017 Dar es Salaam kwa nia ya kudanganya alijitambulisha kama Gerson Msigwa ambaye ni Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu kwa Ladslaus Matindi.


Amedai kuwa mshtakiwa huyo alifanya kosa hilo katika kipindi hicho kwa lengo la kujaribu kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu


Mshtakiwa alikana shtaka upande wa mashtaka ulidai upelezi bado haujakamilika, Mshtakiwa ametakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao watasaini bondi ya sh 1 milioni.Kesi imeahirishwa 23,8,2017 na mtuhumiwa hajakamilisha masharti hayo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post