TUME YA HAKI ZA BINADAMU YAKERWA NA MATAMSHI YA RAIS MSTAAFU BENJAMINI MKAPA

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania imesema imesikitishwa na matamshi ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa.


Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari imesema imesikitishwa na kauli ya rais wa awamu ya tatu akirudia maneno ya kejeli ya watanzania wenye maoni tofauti.


Kwa mujibu wa taarifa hiyo Mkapa alisema akiwa Chato, Geita kuwa Takwimu zilizotolewa na Waziri wa Afya siku hiyo( Julai 10, 2017) ya makabidhiano ya nyumba 50 zilizojengwa na Mkapa Foundaton Zitawasaida kupunguza Upumbavu Wale aliowaita hivyo Wakati wa Kampeni 2015.


Taarifa hiyo imesema kuwa matamshi ya Mkapa hayapendezi kusikika yakitoka kwa kiongozi wa kitaifa, na ni matamshi yasiyoheshimu maoni tofauti.

==>Isome taarifa hiyo hapo chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post