MZEE MWENYE WATOTO 100 ATAKA KUZAA ZAIDI ILI AZIKWE VIZURI AKIFA

Kofi Asilenu mwenye umri wa miaka 80 ni baba wa watoto 100 na wake 12.


Wakati ulimwengu ulipoadhimisha siku ya idadi ya watu duniani mwanaume mmoja alikuwa na sababu 100 za kusherehekea.

Kofi Asilenu mwenye umri wa miaka 80 ni baba wa watoto 100 na wake 12.

Anaishi na familia yake katika kijiji cha Amankrom kilicho umbali wa kilomita 45 kutoka mji mkuu Acca.

Familia yake ni thuluthi moja ya watu 600 katika kijiji hicho.

Anasema kuwa anataka familia kubwa kwa sababu hana ndugu.

Sina kaka wala shangazi,ndiyo sababu niliamua kuwa na watoto wengi ndiyo wapate kunipa maziko yaliyo mazuri nikifa.

Familia hiyo yake hata hivyo imemgharimu pakubwa. anasema alikuwa mtu mwenye mali, lakini mali hiyo ilipungua kutokana na gharama ya kuitunza familia yake kubwa

Kofi Asilenu anaonekama kuwa mwenye afya nzuri na hata anasema anataka kuwa na watoto zaidi.
Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post