MWALIMU WA SEKONDARI MBARONI KWA KUMPA UJAUZITO MWANAFUNZI WAKE


POLISI mkoani Rukwa inamshikilia mwalimu wa Shule ya Sekondari Miangalua iliyopo katika wilaya ya Sumbawanga akituhumiwa kumpatia ujauzito mwanafunzi wake mwenye umri wa miaka 16, ambaye alikuwa akisoma kidato cha tatu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, George Kyando amethibitisha kuwapo kwa tukio hilo, akisema tayari mtuhumiwa huyo amekamatwa na anashikiliwa kwa mahojiano na katika Kituo cha Polisi kilichopo katika mji mdogo wa Laela wilayani Sumbawanga.

Atafikishwa mahakamani mara tu baada ya upelelezi wa awali kukamilika ambapo anatuhumiwa kwa makosa matatu ya kumpatia ujauzito mwanafunzi huo, kumbaka na kukatisha masomo yake.

Akizungumzia mkasa huo, Mkuu wa shule hiyo, Gishi Milundi amekiri kutokea kwa mkasa huo ambapo mwalimu wake anahusishwa na tuhuma hizo huku akiongeza kuwa, baada ya kuhisiwa kuwa ana dalili za ujauzito alikwenda kupimwa katika zahanati ya Miangalua na kubainika kuwa na ujauzito wa miezi mitano.

IMEANDIKWA NA PETY SIYAME, SUMBAWANGA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527