MGANGA WA KIENYEJI AUAWA KWA KUCHOMWA MKUKI


WATU watano wakiwemo watoto wawili wamekufa katika matukio tofauti yaliyotokea mkoani ambapo mganga wa jadi, Levocatus Kanjalanga (65) ameuawa kikatili kwa kuchomwa mkuki mgongoni na mtu asiyefahamika.

Matukio hayo ambayo yametokea katika Wilaya za Nkasi, Kalambo na Manispaa ya Sumbawanga yamethibitishwa kwa nyakati tofauti na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, George Kyando  na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Said Mtanda.

Mtoto wa mganga huyo, Simon Kanjalanga alilieleza kuwa baba yake aliuawa juzi saa moja na nusu asubuhi kwa kupigwa na mkuki mgongoni akiwa anatembea mitaani katika kitongoji cha Chawe kilichopo katika Mji wa Namanyere wilayani Nkasi.

Taarifa kutoka eneo hilo la tukio zinaeleza kuwa mganga huyo wa kienyeji alikuwa akituhumiwa na wateja wake kuwa alikuwa akiwatoza fedha nyingi za matibabu lakini walikuwa hawaponi kupitia uganga wake huo.

Akithibitisha Mkuu wa Wilaya hiyo, Mtanda alieleza kuwa watu wawili wameuawa kikatili wilayani humo akiwemo mganga huyo kwa kile kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina .

IMEANDIKWA NA PETI SIYAME- HABARILEO SUMBAWANGA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527