MBUNGE WA CHADEMA HALIMA MDEE AFIKISHWA MAHAKAMANI KISUTU DAR


Mbunge wa Jimbo la Kawe Halima Mdee amefikshwa katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu leo Jijini Dar es salaam.

Halima Mdee (Chadema), alikamatwa Julai 4 Jioni, na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa na agizo la Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi. Kwa kile kilichodaiwa alitoa lugha ya kumtukana Rais Magufuli.

Pichani ni Mbunge wa Jimbo la Kawe Halima mdee, akiwa amehifadhiwa katika ukumbi wa Wazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akisubiri kusomewa kesi yake. 
Mbunge wa Jimbo la Kawe Halima mdee akisalimiana na Mbunge wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) , Ester Bulaya, akiwa amehifadhiwa katika ukumbi wa Wazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akisubiri kusomewa kesi yake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post