RAIS MAGUFULI AMLILIA MKURUGENZI MKUU WA BENKI YA AFDB ALIYEFARIKI DUNIA GHAFLA AKIWA OFISINI KWAKE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Joseph Pombe Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko mkubwa kifo cha Mkurugenzi Mkuu wa benki ya AFDB Dkt Tonia Kandiero kilichotokea usiku wa jana, na kusema kwamba ni mtu aliyechangia maendeleo Tanzania.


Rais Magufuli ametuma salamu hizo za rambirambi kwa Rais wa benki hiyo Akinwumi Adesina na kusema kuwa Dkt Tonia atamkumbuka kama hodari na mchapakazi katika kipindi cha uhai wake na kwamba kwa kushirikiana kwao kulifanikisha kukamilika kwa miradi mikubwa iliyokuwa chini ya ufadhili wa AFNB.


Kifo cha Dkt Tonia kimetokea usiku wa jana Juni 28 alipokuwa ofisini kwake huko Pretoria Afrika kusini.


==>Hapo chini ni taarifa ya IKULU 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments