WANAFUNZI WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA ARUSHA WAFIKIA 32

Kamanda wa Polisi, mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema wanafunzi 31 na walimu wao wamefariki katika ajali iliyotokea wilayani Karatu, ulipo mto Mlera.
Mkumbo amesema wanafunzi waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni wa shule ya mchepuo wa Kiingereza, iitwayo Luck Vicent ya mjini Arusha.

Kati ya wale waliofariki 28 walikuwa wanafunzi huku watatu wakiwa ni dereva na walimu wao

Ripoti zinasema kuwa basi hilo liliteleza na kukosa mwelekeo ,likatoka katika barabara na kuanguka katika mto katika eneo la Marera eneo la Rhotia, kilomita chache kabla ya karatu katika barabara ya Arusha

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post