NAY WA MITEGO KUACHIA REMIX YA WIMBO 'WAPO'

Msanii wa muziki wa hip hop, Nay wa Mitego amedai remix ya wimbo ‘Wapo’ kwaajili ya Rais John Pombe Magufuli iko tayari na inaweza kuachiwa muda wowote.


Rais Magufuli aliufungulia wimbo huo baada ya kufungiwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kigezo cha maadili na kumtaka rapa, Nay wa Mitego kuongeza baadhi ya maneno katika wimbo huo ili uwaguse watu wengi zaidi.

Nay wa Mitego amedai remix ya wimbo huo iko tayari na ameongeza vitu vingi ndani ya wimbo huo.

“Kusema kweli wimbo wa Mh Rais umekamilika na muda wowote unaweza kutoka.

“Nimeongeza mambo mengi ndani yake, kwahiyo mashabiki wakae mkao wa kula kwaajili ya moto mwingine kwa sababu bado ‘Wopo’ yenyewe inaendelea kufanya vizuri,”

Rapa huyo amedai hawezi kusema ni lini project hiyo itatoka.

Katika hatua nyingine rapa huyo amewataka mashabiki wa muziki wake kuendelea kumuunga mkono katika muziki wake pamoja na kujitokeza kwa wingi katika tour yake ya ‘Wapo’ ambayo imeingia ndani ya jiji la Dar es salaam.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post