DIAMOND PLATNUMZ KUHUDHURIA MAZISHI YA MUME WA ZAMANI WA ZARI?

Mwanamuziki,Diamond Plantinumz  alikuwa  nchini Kenya kwa ajili ya tamasha la Koroga ambalo lilifanyika jana  Jumapili Mei 28,2017


Diamond aliwahutubia wanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi na kuzungumzia kifo cha aliyekuwa mme wa mkewe wa sasa, Ivan Ssemwanga

Ssemwanga alifariki akiwa amelazwa katika hospitali moja nchini Afrika Kusini baada ya kukumbwa na mshtuko wa moyo
****
Mwanamuziki, Diamond Plantinumz amezungumzia kifo cha aliyekuwa mme wa mkewe ,Zari Hassan ambaye alifariki juma lililopita akipokea matibabu katika hospitali moja Afrika kusini.

Akizungumza akiwa katika chuo kikuu cha Nairobi Ijumaa Mei 26, Diamond alisema kuwa Zari anapitia wakati mgumu ikizingatiwa kuwa alizaa watoto watatu na Ssemwanga .

Aidha ,Diamond alisema kuwa hangekosa kwenda Kenya kuhudhuria tamasha la Koroga kwa sababu alikuwa tayari amewaahidi Wakenya kwamba angeenda kabla ya msiba huo kutokea.

Diamond alisema atahudhuria mazishi ya mwenzake,Ssemwanga.

"Kwa kweli umekuwa ni wakati mgumu kufutilia mbali mualiko huu. Nimeongea na mke wangu akanielewa. Nikimaliza hapa nitaenda Uganda kwa sababu ya mazishi," Diamond alisema.

Marehemu Ivan Ssemwanga alikuwa amemuoa Zari Hassan ambaye kwa pamoja walikuwa na watoto watatu wa kiume kabla ya kutalakiana kisha Zari akaolewa na Diamond.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527