NB- Pichani ni mfano wa kiberenge |
Mashuhuda wa tukio hilo wameiambia Malunde1 blog kuwa mwanamke huyo alikuwa amepanda kwenye pikipiki akielekea kusali kwenye mkesha wa Pasaka katika kanisa katoliki Bugisi.
"Alikuwa amepakizwa kwenye bodaboda,mwendesha bodaboda alikuwa anakatisha relini bila kuchukua tahadhari ghafla wakaona kiberenge kikija,mwendesha bodaboda akaongeza mwendo na kuvuka reli...mwanamke huyo akaruka kwenye pikipiki na kuangukia relini kisha kusagwa na kiberenge hicho",wameeleza mashuhuda wa tukio hilo.
"Mwanamke huyo ambaye ni mke wa mwalimu wa shule ya msingi Mwanono alikuwa anakwenda kusali kanisa la Bugisi".
Tutawaletea habari kamili hivi punde...Endelea Kutembelea Malunde1 blog,Fahari ya Shinyanga
Social Plugin