RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA ELIMU

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha Dkt. Crispin Mpemba ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma za kiutendaji zinazomkabili ikiwemo uendeshaji wa shirika hilo

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene amesema moja ya tuhuma zinazomkabili ni pamoja na kuingia mikataba kiholela.

Shirika la Elimu Kibaha ni Shirika la umma linalotoa huduma mbalimbali likiwa na ofisi zake Mkoa wa Pwani kilomita 40 Magharibi mwa Mji wa Dar es salaam.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post