KESI YA WEMA SEPETU DAWA ZA KULEVYA YAPIGWA KALENDA

Kesi ya Dawa za kulevya inayomkabili muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu iliyokuwa isikilizwe leo, imeahirishwa hadi Aprili 11 mwaka huu baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa upelelezi haujakamilika.


Muigizaji huyo ni mmoja kati ya wasanii ambao walitajwa kwenye list ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda yawatuhumiwa wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.


Katika upelelezi wa awali ambao ulifanywa na jeshi la polisi, walidai wamekuta msokoto wa bangi nyumbani kwa muigizaji huyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post