KIGWANGALLA: KUTANGAZA MAJINA YA MASHOGA HADHARANI NI SAWA NA KUFUNGULIA JINI LILILOWEKWA KWENYE CHUPA"

Leo February 27 2017 Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilikuwa na mpango kuwa na Mkutano na Waandishi wa habari ulioandaliwa kuwataja Watanzania wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kujiuza mitandaoni lakini baadae leo Mkutano huo uliahirishwa.

Baada ya kuahirishwa kwa mkutano huo, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameandika kupitia account yake ya twitter haya……
“Kwa orodha tuliyonayo, kutangaza majina ya mashoga hadharani, ni sawa na kufungulia jini lililowekwa kwenye chupa!”-Kigwangalla.
“Kwa sababu za kimkakati, na ili kuepuka kuharibu ushahidi, tutalishughulikia jambo hili kwa namna nyingine, tutawajulisha matokeo kila hatua”-Kigwangalla.

Via>>Millardayo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527